Mawaziri kutoka maeneo mbalimbali duniani wanakutana
katika makao ya umoja wa mataifa mjini Vienna kuzungumzia njia za
kupambana na dawa za kulevya.
Tume ya kimatifa inayoshugulikia dawa za kulevya inatarajiwa kutoa taarifa ya pamoja.
Hata hivyo kumetokea mgawanyiko kati
ya...
nchi ambazo zinataka sera za dawa hizo kuzingatia zaidi maswala ya
afya ya umma na nyingine kama Iran,Pakistan na Uchina ambazo zinataka
kusalia na adhabu kali kwa wanaoshiriki biashara ya dawa za kulevya.
Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwepo mabadiliko muhimu kuhusu udhibiti wa dawa za kulevya duniani.
Mwezi Disemba Uruguay ikawa nchi ya kwanza
kuhalalisha bangi, na baadaye majimbo ya Marekani ya Washington na
Colorado yakafuata. Baadhi ya nchi za Amerika ya kusini zimetangaza kuwa
vita dhidi ya dawa za kulevya vimefeli.
Lakini Baadhi ya nchi zinatoa wito kuwepo sera mpya zitakazozingatia afya ya umma na kuzuia matumizi mabaya ya dawa za kulevya.
Kuna pia baadhi ya nchi kama Iran Pakistan na
Uchina ambazo zinataka kuwepo adhabu kali kwa wanaofanya biashara ya
dawa za kulevya ikiwemo hukumu ya kifo.
Mkutano wa Vienna unatarajiwa kutoa taarifa ya pamoja lakini ni wazi kuwa kumeibuka tofauti. |
0 comments:
Post a Comment