Timu ya soka ya Ivory Coast huenda
ikakabiliwa na vikwazo baada ya mashabiki wake kuvamia uwanja mjini
Abidjan baada ya kupata fursa ya kuwakilishwa katika michuano ya mataifa
ya bara Afrika.
kisa hicho kilitokea baada ya timu hiyo kupata
sare ya bila kwa bila dhidi ya Cameroon siku ya jumatano ili kuhakikisha
kuwa wanamaliza wa pili katika kundi Da.Shrikisho la soka barani Afrika CAF limesema kuwa linasubiri ripoti ya refa kuhusu kisa hicho.
Kisa hicho huenda kikaangaziwa na kamati ya maandalizi mnamo tarehe mosi mwezi Disemba.
0 comments:
Post a Comment