Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema hadhani ni
sawa kurejesha fedha za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake binafsi
kwa sababu hakuwahi kutoa pendekezo hilo.
Bw. Zuma amesema haoni haja ya kuchangia pesa
zake binafsi katia ukarabati wa nyumba hiyo kwani halikuwa pendekezo
lake toka mwanzoni.Kadhalika bwana Zuma ameambia runinga moja nchini Afrika Kusini kwamba maafisa wa serikali ndio waliopanga ukarabati huo uliogharimu dola milioni 23 bila kumuarifu.
Hii ndio mara ya kwanza Rais Zuma kuzungumzia kuhusu...
makaazi hayo yaliyozua mjadala mkali wa umma Afrika Kusini.
Mhifadhi wa mali ya umma alisema baadhi ya ukarabati uliofanywa sio halali na kumtaka Zuma kurejesha baadhi ya fedha zilizotumika.
0 comments:
Post a Comment