Friday, March 21, 2014
0
Polisi watatu wanaolinda makazi ya waziri mkuu wa Pakistan wamesimamishwa kazi kwa muda baada ya Paka kumuua Tausi wa waziri mkuu.
Mtunza bustani alikuta Tausi mmoja....
amekufa katika moja ya bustani za makazi ambapo ndege hao huvinjari , lilieleza gazeti la Express Tribune.
Mmoja wa maafisa waliosimamishwa kazi amesema wengine 21 waliitwa kujieleza baadae. Imeripotiwa kuwa maafisa hao walisema walikuwa kazini usiku ule , lakini hawakutegemea kuwa Paka wangemla Tausi.
Maafisa 18 hawakubainika kuwa na hatia, gazeti lilieleza.
Lakini watatu waliosalia wote walipewa onyo na kuadhibiwa kwa uzembe
Makazi ya waziri mkuu wa Pakistani Nawaz Sharif yako Raiwind, viungani mwa mji wa Lahore.
SOURCE BBC

0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA