Thursday, March 06, 2014
0
Serikali ya Libya imesema kuwa mtoto wa Kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, Saadi Gaddafi, ameondoshwa nchini Niger na  hivi sasa....
anashikiliwa mjini Tripoli.
Saadi alitoroka baada ya baba yake, Kanali Muammar Gaddafi kuuawa wakati wa mapinduzi yaliyofanyika mwaka 2011 nchini Libya.
Anashutumiwa kuwafyatulia risasi waandamanaji na anadaiwa kutekeleza uhalifu mwingine wakati wa utawala wa baba yake, yeye alipokuwa Kiongozi wa vikosi maalum vya kijeshi.
Serikali ya Libya imetoa taarifa hiyo mapema siku ya alhamisi kuwa wamempokea akitokea Niger.
awali , Niger ilikataa ombi la Libya ilipotaka imsafirishe Saadi, huku waziri wa sheria wa Niger akihofu kuwa Saadi atahukumiwa adhabu ya kifo.
SOURCE:BBC SWAHILI

0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA