Mahakama nchini Ujerumani imemhukumu rais wa klabu
bingwa Ulaya, Bayern Munich, Uli Hoeness, kifungo cha miaka mitatu na
miezi sita jela kwa kukwepa kulipa kodi.
Nyota huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 62
alikiri kuitapeli mamlaka ya...
kutoza ushuru ya Ujerumani mamilioni ya
Euro huku akiweka akiba ya fedha zake kisiri kwenye akaunti ya benki ya
Uswizi.
Licha ya wakili wake kuiomba
mahakama kutomwadhibu Bw Hoeness kwa sababu ya kujisalimisha kwake,
mahakimu waliafikia kwamba Hoeness hakukiri kikamilifu.
Hapo awali Hoeness alishtakiwa kwa kukwepa
kulipa ushuru wa euro milioni 3.5 (£2.9m; $4.9m) lakini baadaye akakiri
kuwa hajawahi kulipa milioni nyingine 15.
Hatimaye Alhamisi, korti ilibaini kuwa alikosa kulipa ushuru wa jumla ya euro milioni 27.2.
Hoeness amesema hatakata rufaa dhidi ya uamuzi huo
Hata hivyo Hoeness atabakia kuwa huru hadi uamuzi wa mwisho kabisa utakapotolewa. |
0 comments:
Post a Comment