Teodorin Obiang anadaiwa kupora mali ya umma na kujinunulia majumba na magari ya kifahari Ufaransa
Uchunguzi umeanzishwa rasmi dhidi ya mwanawe Rais wa Equatorial Guinea,Teodorin Obiang nchini Ufaransa.
Teodorin Obiang anadaiwa kupora mali ya umma na.... kujinunulia majumba na magari ya kifahari Ufaransa
Obiang anatuhumiwa kwa kosa la kujipatia pesa kwa njia haramu.
Mahakimu nchini Ufaransa wamekuwa wakiendesha uchunguzi dhidi ya viongozi wa nchi hiyo tangu mwaka 2010.
Wengi wanadaiwa kuhusika na uporaji wa pesa za
umma huku wakijinunulia mali nyingi katika nchi za kigeni hususan nchini
Ufaransa.
Bwana Teodorin Obiang amekana kuhusika na wizi
akisema kuwa mali yake ambayo imemuwezesha kununua nyumba ya kifahari
mjini Paris ,ndege ya kibinafsi na magari ya kifahari ameipata kwa njia
halali.
Pia anakabiliwa na tuhuma za wizi wa pesa nchini Marekani.
0 comments:
Post a Comment