siku zingine wakitembea kwa miguu katika mji mkuu Paris.
Hali ya ukungu unaotanda kote Paris ni kutokana na hali ya baridi kali usiku na mchana jambo linalozuia hewa kuchanganyika vyema.
Mnamo siku ya Ijumaa serikali ilitoa usafiri bila malipo kwa wananchi ili kuwashashwishi kuacha kutumia magari yao. Hali hiyo itaendelea siku ya Jumatatu.
Wanasayansi wanasema kuwa uchafuzi wa mazingira mjini Paris umekuwa mbaya sana hata kuliko mji wa Beijing wenye mazingira chafu zaidi ya hewa duniani.
Mnamo siku ya Ijumaa, kiwango cha uchafuzi wa mazingira kilikuwa kikubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Serikali itatathmini viwango vya uchafuzi siku ya Jumatatu na kuona ikiwa itaongeza muda wa agizo hilo au la.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.