Kamati inayohusika na sera za fedha imesema hela hiyo iliyobaki inaweza kununua bidhaa muhimu kutoka nje ya nchi kwa mahitaji ya mda wa miezi minne pekee.
Mwaka 2011 Swaziland iliiomba Afrika kusini msaada wa dharura baada ya kuishiwa na hela.
Swaziland ilipiga marufuku vyama vya kisiasa nchini humo tangu 1973 na imeshtumiwa kwa rekodi yake mbaya ya uvunjaj wa haki za binadamu. Wakereetwa wa kupigia kampeni mageusi ya
ki-democrasia mara nyingi hukamatwa na kushtakiwa kwa ugaidi kisha kuzuiliwa magerezani.
Mfalme Mswati na familia yake wameshtumiwa kwa ubadhirifu na ufujaji wa fedha huku wengi wa raia wa Swaziland wakibaki kuwa miongoni mwa maskini zaidi duniani.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.