Twiga wote wawili walipelekwa kufanyiwa uchunguzi lakini chombo cha serikali kinachozuia ukatili juu ya wanyama kimesem mmoja alikufa mara tu baada ya kufikishwa katika eneo la matibabu.
Tukio hili limezua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.
Shuhuda, Thinus Botha aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa Twitter kuwa alikuwa akiendesha nyuma ya Lori hilo akashuhudia namna Twiga huyo alivyojigonga kwenye Daraja la Garsfontein barabara ya N1 ya Johannesburg's.
Kulikuwa na damu nyingi, Thinus Botha aliandika.
Meneja wa chombo cha serikali kinachozuia ukatili juu ya wanyama Afrika ya Kusini, alikuwa amejeruhiwa kichwa chake lakini uchunguzi unapaswa kufanyika kujua chanzo cha kifo.
Amesema pia wanyama hao walikuwa wakisafirishwa kuelekea bustani ya wanyama iliyoko Warmbarths, kama Kilomita 160 yaani maili 99 nje ya Johannesburg.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.