Klabu hiyo kwa jina, Clermont, ilisema kuwa kocha mpya Helena Costa, aliyekuwa kocha wa timu za taifa za wanawake nchini Qatar na Iraq, ataanza kazi msimu ujao.
Costa pia aliwahi kuwa afisa wa klabu ya Celtic nchini Scotland ambaye kazi yake ilikuwa kuwatafuta wachezaji chipukizi wenye kipajii cha juu kuchezea klabu hiyo.
Pia aliwahi kuwa kocha wa timu ya wanawake ya Iran tangu mwaka 2012.
Klabu ya Clermont imesema kuwa ina matumaini makubwa kwamba Helena atasaidia klabu kupiga hatua.
Atachukua nafasi ya Regis Brouard, ambaye mkataba wake unakamilika mwishoni mwa msimu.
Klabu hiyo inashikilia nafasi ya 14 katika ligi ya daraja ya pili.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.