Msemaji wa Polisi nchini Nepal amesema kuwa serikali ya taifa imewatuma wakufunzi 600 wa maswala ya tabia na uhusiano mwema katika majimbo yote nchini humo kujaribu kuboresha uhusiano baina ya maafisa wa polisi na umma.
Kampeini hiyo imepewa jina la "huduma na tabasamu"na inanuiwa kufuta kumbukumbu ya uhusiano baina ya polisi na umma wakati wa vita vya wenyewe kwa wenye nchini humo.
Msemaji wa polisi KC Ganesh amesema kuwa maafisa 67,000 katika wilaya 75 ya Nepal wamelengwa katika kampeini hiyo mpya.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.