Maafisa nchini Australia, China na Malaysia, watakutana mjini Canberra wiki ijayo, kujadili juhudi za kusaka mabaki ya ndege hiyo ambazo bado zinaendelea
Mnamo siku ya Alhamisi, kulikuwa na taarifa kwamba ndege ya MH370 ilianza kutafutwa baada ya saa nne za kupotea kwake.
Ripoti ya hapo awali kutoka kwa waziri wa usafiri wa Malysia, pia ilisema kuwa wahudumu wa trafiki ya ndege, hawakugundua kuwa ndege hiyo ilitoweka hadi dakika kumi na saba baada ya kukosa kuonekana katika mtambo wa Radar.
Ndege hiyo ilikuwa imewabeba watu 239 ilipotoweka ikiwa katika anga ya kusini mwa bahari ya China njiani kuelekea Beijing.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.