Bi Esther Rantzen mwanzilishi wa huduma hiyo Silver Line, anasema kiwango hicho kikubwa cha wapigaji simu ni dhihirisho halisi la tatizo la upweke linalokumba wengi wa wazee katika mfumo wa kisasa wa maisha nchini Uingereza.
Nusu wa waliopiga simu wamesema wanaeza kukaa kutwa bila kuzungumza na mtu , ilhali mmoja kati ya kumi wakasema huchukua hata zaidi ya wiki nzima bila kupata mtu wa kuzungumza nao.
Utafiti wa kisaikolojia wasema upweke mwingi unaeza kuleta madhara kama vile majonzi, msongo wa mawazo na athari nyenginezo za kiafya na hasa kiakili.
Tahadhari imetolewa kwa nchi zinazoendelea hasa barani Afrika kufanya jitihada kuzuia mmomonyoko wa kimaadili na utamaduni wa kutunza wazee ili kuepukana na hali kama hiyo.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.