Maafisa wa utawala walisema kuwa wataweza kuwapa mikataba watu watakaoteuliwa kushiriki katika zoezi la kuwapiga risasi Nguruwe wanaorandaranda mjini humo, kulingana na malipo watakayotaka.
Waliongeza kuwa wale watakaoruhusiwa kuwaua Nguruwe hao watateuliwa mwezi Mei.
‘‘Huu ni unyama na sio suluhu la tatizo la wanyama hao wanaorandaranda mjini,’’alisema Puneet Tripathi, mwasisi wa shirika la kutetea haki za wanyama na mazingira.
‘‘Lazima maafisa waangalie njia nyengine za kusuluhisha tatizo hilo labda kwa kuwahamisha wanyama hao hadi katika mji mwingine,’’ aliongeza bwana Puneet.
Baadhi ya wanaharakati wanasema kuwapiga risasi Nguruwe itakuwa kinyume na sheria za India kuhusu ukatili.
Nguruwe wameonekana kama kero sio mjini humo pekee bali pia katika miji mingine nchini India. Huonekana mara kwa mara wakipekuwa kwenye majaa ya taka wakitafuta chakula.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.