Jaji huyo amewashauri wakenya kutumia wazee wa vijiji, makanisa na miskiti kutatua migogoro na kusema kuwa yeye binafsi amewaambia watu wa jimbo la Kitui anakotoka
kuwatembelea wachawi na waganga kutatua baadhi ya...
masuala yao.
Jaji mkuu aliyasema haya akiwa Gatundu katika eneo la kati alipokuwa akifungua mahakama mapya ya Kiambu.
Amesema kuwa huduma za mahakama ni ghali mno na akatoa wito kwa wanaotafuta haki mahakamani haswa kuhusu maswala ya familia, kutumia vikao vingine huku akiongeza kuwa mfumo wa kisheria
Uchawi
"kusema tukutane kortini ni upumbavu mtupu kwa sababu pesa zenu zitaliwa na mawakili. afadhali muende kwa wazee au kwa viongozi wa kidini"
Amesema kuwa katiba, inaruhusu watu kutumia njia mbadala kutatua migogoro badala ya kutumia masaa mengi na kiasi kikubwa cha fedha kwa mawakili .
Kipengee cha 159 ya Katiba ya Kenya inawaruhusu wakenya kutafuta njia mbadala za kusuluhisha ubishi miongoni mwao.
Kesi zaidi ya 600,000 zipo kortini zikisubiri kuamuliwa na kulingana na jaji mkuu wa Kenya asilimia kubwa ya kesi hizi zinaweza suluhishwa nje ya mahakama.
Katika utamaduni wa Kiafrika ubishi mwingi ulikuwa unaamuliwa na wazee lakini maamuzi yao haswa katika maswala mengine kama vile ubakaji uhalifu na mauaji yakasababisha serikali kuingilia kati
kwa kuwafikisha watuhumiwa mahakamani na hivyo ikapunguza hadhi ya vikao hivyo vya wazee miongoni mwa wakenya.
Katika sehemu nyingi nchini Kenya waganga na madaktari wa kienyeji huwa wanatumika kuwanasa wezi na washukiwa wa uhalifu.
Hata hivyo,kumetokea idadi kubwa ya watu wanaonadi huduma zao katika maeneo ya miji na kushukiwa kuwa ni walaghai tu kutokana na idadi kubwa ya magonjwa wanayodai kutibu ikiwemo
magongwa ambayo hayana tiba kama vile Ukimwi .
Hoja yake tayari imezua mjadala mkubwa nchini Kenya ,Kiongozi wa Serikali bungeni Adan Duale ,akimpuzilia mbali na kudai kuwa hiyo ni dalili kuwa ameshindwa na majukumu yake .
Idara ya mahakama nchini Kenya imelaumiwa kwa kushindwa kutoa uamuzi wa kesi haraka na kupelekea watu wengi kukata tamaa ya kupata suluhu baada ya kesi zao kutoamuliwa kwa zaidi ya
miaka 5 hadi miaka kumi.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.