Mwanamume mmoja aliyeishi jela kwa zaidi ya miaka 25
akisubiri hukumu ya kifo nchini Marekani, ameachiliwa huru baada ya
mahakama kubatilisha uamuzi wa mahakama kuwa alikuwa na hatia ya mauaji
yaliyotokea mwaka 1983.
Glenn Ford, 64, alikuwa jela akisubiri hukumu ya kunyongwa tangu..mwaka 1988 mwezi Agosti.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa ni mmoja wa wafungwa waliohukumiwa kifo kwa muda mrefu nchini humo na kuachiliwa.
Glenn alisema kuwa anahisi vizuri sana kwamba ameachiliwa.
Makosa kwenye kesi
- Hakuna silaha yoyote ilipatikana na hapakuwa na mashahidi katika kesi hiyo.
- Mwanamke aliyemhusisha Ford na mauaji hayo alisema kuwa ushahidi wake haukuwa wa kweli na kwamba alidanganya.
- Mawakili wa Ford walioteuliwa na mahakama hawakuwahi kuendesha kesi ya mauaji
- Bwana Mmarekani mweusi alihukumiwa na jopo la wazungu waliopendekeza auawe.
"miaka 30 ya maisha yangu. Siwezi kufanya mambo ambayo ningefanya nikiwa na umri wa miaka 35, 38 au 40. Mwanangu nilipofungwa jela alikuwa mtoto sasa ni mtu mzima na watoto wake.''
Jaji aliymwachilia huru bwana Ford, Ramona Emanuel alisema Jumatatu kuwa kulikuwa na ushahidi mpya kuonyesha kwamba Bwana Ford, hakuhusika na mauaji hayo.
Makosa mengi yalipatikana katika kesi dhidi ya Ford kama yalivyoelezwa na vyombo vya habari nchini Marekani.
Inaarifiwa kuwa kesi ya Ford iliendeshwa na mawakili ambao hawakua na ujuzi wa kazi.
SOURCE BBC SWAHILI
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.