Friday, April 18, 2014
0

Mamake mwathiriwa alimzaba kofi mtuhumiwa na kisha kumasamehe dakika chache kabla ya kunyongwa


Mtu mmoja aliyehukumiwa kifo kwa kunyongwa nchini Iran baada ya kupatikana na hatia ya mauaji, ameponea chupuchupu baada ya kusamehewa na mamake mwathiriwa.
Mama huyo alimsamehe mtuhumiwa dakika chache tu kabla ya kuwekwa kamba shingoni.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Iran.
Picha za tukio hilo zilipigwa moja kwa moja na mpiga picha mmoja aliyenasa kila hatua ya tukio hilo ambalo liliwashangaza wengi nchini Iran na......
duniani kote.


Balal alimuua kwa kumdunga kisu Abdollah Hosseinzadeh miaka saba iliyopita

Shirika la habari la ISNA nchini Iran liliripoti kuwa mtuhumiwa huyo, kwa jina Bilal, alihukumiwa kifo baada ya kumuua kijana mmoja Abdollah Hosseinzadeh, wakati wawili hao walipokuwa wanapigana katika soko moja mjini Nour miaka saba iliyopita.
Bilal alifikishwa katika sehemu ya kunyongewa akiwa amefunikwa macho yake tayari kwa hukumu kutekelezwa siku ya Jumanne.
Lakini dakika ya mwisho kabla ya kunyongwa, mamake mwathiriwa Samereh Alinejad, alimwambia kuwa amemsamehe baada ya kuhutubia umati uliofika kushuhudia hukumu hiyo , kisha akamzaba kofi Bilal kabla ya Bilal kunusurika kifo.

0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA