Saturday, April 12, 2014
0
Mwanamume mmoja aliyekuwa mfanyakazi wa benki nchini Uingereza, amefungwa maisha jela kwa kumuua mke wake.
Jasvir Ginday aliambia mahakama kuwa alimuua mkewe baada ya kumtishia kuwa angewaambia wazazi wao kuwa mume wake hushiriki mapenzi ya jinsia moja.
Jasvir Ram Ginday, mwenye umri wa miaka 29, alimshambulia mareemu mkewe Varkha Rani kwa chuma ya mashine ya kusafisha nyumba.
Mahakama ilisikia Ginday alivyomnyonga mkewe na kisha kuchoma mwili wake.
Harusi ya wawili hao ilikuwa harusi ya kupangwa
Jaji John Warner alisema kuwa Ginday alikuwa na wakati mgumu kama mwanamume anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja hasa kwa....
kuwa aliishi katika jamii ya watu wasiokua kama yeye.
Kesi hii ilisikikilizwa kwa wiki tatu.
Harusi ya wawili hao ilifanyika baada ya Ginday kuja London kutoka nchini India kukutana na mkewe katika harusi yao ya kupangwa.
Lakini alikuwa amemwambia rafiki yake mwaka 2008 kuwa yeye huvutiwa zaidi na wanaume licha ya kwamba alikuwa anamuoa mchumba wake Varkha aliyekuwa na miaka 24.
Jasvir Ginday
Polisi waliambia mahakama kuwa Ginday alizoea kuzuru baa za watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kwamba alizoea sana kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume wengi.
Wakati kesi ilipokuwa ikiendelea, Ginday alidai kuwa mkewe alitishia kufichua kwa familia zao kuwa aliozwa mwanamume ambaye hushiriki mapenzi ya jinsia moja baada ya kupata picha chafu kwenye simu yake.
Aliambia mahakama kuwa baada ya mkewe kupata picha hizo alikimbia chumbani na kumtishia na hapo ndipo alipomgonga na chuma kichwani na kumuua kutokana na hasira.
Aliwadangaya wazazi wake kuwa mkewe alimuacha lakini baada ya uchunguzi kufanywa polisi walipata fuvu la kichwa katika nyumba yao.

0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA