Amini
usiamin. Bodi la gari hili aina ya Hiace lenye namba za usajili T921
BME limetengenezwa kwa mbao aina ya mlingoti na pine. Linamilikiwa na mvunaji na mfanyabishara wa mbao wa Nyololo, Mafinga, mkoani Iringa Bw.Kenny Mwangoka.
Mwangoka alilinunua gari hilo lililokuwa linamilikiwa na mission ya
kanisa katoliki Mafinga baada ya kupata ajali na kuharibika
vibaya. Jitihada zake za kulifufua gari hilo kwa kuvisha bodi mpya
hazikuzaa matunda na ndipo alipotumia ubunifu huu.
"Sasa nalitumia kuhamasisha utalii, hasa utalii wa mazingira nikiwa na
maana kwamba tukiyatunza mazingira yatatufaa kwa mambo mengi ikiwa ni
pamoja na matengenezo ya magari kama hili langu," anasema, na kuongeza
kuwa atalipeleka kwenye maonesho ya nanenane mwaka huu kama moja ya
njia za kuhamasisha upandaji wa miti.
Na Francis Godwin, Iringa
0 comments:
Post a Comment