Umati mkubwa wa watu wamekusanyika mjini Vatican
kushuhudia tukio la kihistoria ambapo viongozi wawili wa zamani wa
Kanisa Katoliki, Papa John Paul II na Papa John XXIII wametangazwa
watakatifu.
Ibada iliyoendeshwa kwa pamoja kati ya Papa
Francis na mtangulizi wake Papa Benedict XVI imeangaliwa na karibu
mahujaji milioni moja na wengine mamilioni ya watu kupitia matangazo ya
televisheni na redio.
Karibu ujumbe wa wageni 100 wamehudhuria sherehe hiyo, wakiwemo kutoka koo za kifalme na wakuu wa nchi na serikali.
Hii ni mara ya kwanza kwa papa wawili kutangazwa kwa wakati mmoja kuwa watakatifu.
Waandishi wa habari wanasema hatua hii
inachukuliwa kama njia ya kuziunganisha kambi mbili za wapenda mageuzi
na wasiotaka mabadiliko ya sheria katika Kanisa Katoliki.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.