Bwana Di Rupo alikuwa anahutubia kongamano la viongozi wa Afrika na Muungano wa Ulaya mjini Brussels Ubelgiji lililohudhuriwa na Marais wa Afrika.
Mwaka huu Nigeria na Uganda zilikaza sheria zake kuhusu....
mapenzi ya jinsia moja.
Nchini Uganda yeyote anayepatikana na hatia ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja watafungwa maisha jela
Bwana Di Rupo ni afisa wa pili wa ngazi ya juu Ulaya kutangaza kuwa yeye ni shoga. Waziri mkuu wa Ieceland Johanna Sigurdardottir pia amejitangaza kushiriki mapenzi ya jinsia moja.
"hatuwezi kukubali kuwa baadhi yetu wananyimwa haki zao na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa wapenzi wa jinsia moja,'' alisema waziri mkuu huyo
Rais Museveni na mwenzake wa Nigeria Goodluck Jonathan hawajajibu kisomo hicho.
Maafisa wakuu wa Uganda wamekuwa wakitetea msimamo wa Rais Museveni kuhusu sheria yake kali ya mapenzi ya jinsia moja wakisema kuwa Uganda ni nchi huru ambayo mataifa ya magharibi hayawezi kuishawishi hivi hivi.
SOURCE:BBC SWAHILI
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.