Friday, May 23, 2014
0
Mkwezi wa milima mirefu ameokolewa kutoka futi 80 bondeni alipoandika ''Nahitaji msaada'' katika mtandao wa Facebook
Profesa huyo wa jiografia aliwaambia marafiki zake wa Facebook kuwa alikuwa ameanguka ndani ya bonde la Himalaya umbali wa futi 19,600 kwenda chini.
Profesa John All aliandika taarifa hii kwenye ukurasa wa facebook wa ‘'American Climber Science Program’' baada ya kuanguka kwendye bonde hilo. All mwenye umri wa miaka 44 aliteguka bega, kuvunja mbavu tano, goti, na kiwiko.
All aliandika, ‘’ tafadhali muwafahamishe waokoaji wa Global, John amevunjika mkono, mbavu na huenda anavuja damu ndani ya mwili. Tafadhali harakisheni’’
Marafiki wake wa Facebook waliona video ya All akiwa na majeraha na kuwajulisha waokoaji kilichokuwa kikitendeka na kisha kuwasisliana na All na kumwambia kuwa atapata msaada.
Baada ya saa kadhaa, All aliandika kwenye ukurasa huo wa Facebook kuwa waokoaji hawangeweza kumpata kwa kutumia helikopta kwa hivyo angejitahidi ingawa kulikuweko na baridi na alikuwa na maumivu mengi.
Baada ya saa 19, profesa All aliokolewa na kupelekwa hospitalini mjini Kathmandu ambako anapata matibabu.

0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA