Papa Benedict wa kumi na sita,
ametoa baraka zake kwa lugha ya kiarabu katika hotuba yake ya kila wiki kwa
dunia nzima.
Hotuba hiyo hupeperushwa moja kwa
moja kupitia televisheini.
Papa alisema kuwa anawaombea watu
wote wanaotumia lugha ya......
Kiarabu.
Kabla ya maombi yake, padri mmoja
pia alisoma hotuba ya wiki kwa mara ya kwanza katika lugha ya Kiarabu.
Maafisa katika makao makuu Vatican
walisema kuwa hatua hiyo huenda itawafarijji wakristo Mashariki ya kati , wengi
wao ambao wamekuwa wakiondoka kutoka eneo hilo wakisema kuwa wanahofia usalama
wao.
|
0 comments:
Post a Comment