Thursday, August 07, 2014
0


Mwanamke mmoja nchini India ameogelea kwenye mto uliokuwa umejaa maji mengi yaliyotokana na mvua kubwa ilhali akiwa na ujauzito wa miezi tisa.
Anasema sababu ya safari yake majini ni ili aweze kufika katika kituo cha afya aweze kujifungulia hospitalini.
Mama huyo kwa jina Yellawa alitumia maboga makavu yenye maganda magumu yaliyomsaidia kuogelea kwa umbali wa karibu kilomita moja kutoka kwenye kijiji chake kusini mwa jimbo la Karnataka.
Alishikwa na uoga lakini alitaka kujifungua salama, hakuna kituo cha afya kijijini kwake na hakutaka kujifungulia nyumbani.
Wanakijiji na madaktari wamesifu hatua yake ya kuogelea kuwa ni mafanikio makubwa.
Yellawa ni binti wa miaka 22, kutoka kijiji cha Neelakantarayanagadde, kijiji kidogo kando kando ya mto Krishba kaskazini mwa mji wa Bangalore.
Namna pekee ya kusafiri kutoka katika kijiji hicho kwa kuvuka mto ni kwa kutumia miti iliyotengenezwa kwa kuunganishwa mithili ya boti, kifaa ambacho hata hivyo si imara na hakifanyi kazi nyakati ambazo mto huwa umejaa maji.
Wakati Yellawa akiogelea kuvuka mto juma lililopita, maji yalikua yameongezeka ambapo alishuhudia waogeleaji wakisita kuingia kwenye maji.
Binti huyu alishikwa na hofu lakini alijipa moyo kuwa anafanya vile kwa usalama wa mtoto wake.
Yellawa alisaidiwa na baba yake, kaka na ndugu zake ambao waliogelea pamoja naye.
Ingawa alikua amechoka lakini daktari aliyekuwa akimchunguza alipowasili katika hospitali ya serikali karibu na kijiji cha Kekkera alisema kuwa anaendelea vizuri na yuko nyumbani kwa nduguye amepumzika.
Yellawa anasifiwa kwa ushujaa wake wa kuvuka mto kwa hali ya ujauzito aliokuwa nao

0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA