Miili ya wtu waliouwawa na wapiganaji wa "BOKO HARAM" huko Nijeria |
Miili ikiwa barabarani.. |
Nisipojilinda mwenyewe nani atanilinda..? |
Wapiganaji wa boko haram! |
Wanalipua makanisa na nyumba za wakristo! |
Mh. Rais hivi ndivyo hali ilivyo! |
Amri
ya kutotembea usiku imetangazwa katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Kogi
katikati mwa Nigeria baada ya watu wenye silaha kuwaua waumini 19 katika
kanisa.
Watu
hao walivamia kanisa karibu na jiji la Okene jimbo la Kogi na kuwafyatulia
risasi waumini wakati wa ibada siku ya Jumatatu.
Gavana
wa Kogi Idris Wada amesema wauaji hao aliowaita wa kishetani watakamatwa.
Haijafahamika
ni nani aliyehusika na mashambulizi hayo, lakini kundi la kiislamu lenye
msimamo mkali la Boko Haram limekuwa likifanya mashambulizi kadhaa katika
makanisa na maeneo mengine nchini Nigeria.
Mwandishi
wa BBC Chris Ewokor aliyetembelea eneo lililoshambuliwa anasema, eneo hilo liko
tete na kuna uwepo mkubwa wa vikosi vya usalama.
Ushambuliaji
huo umewastua wakristo na waislamu wa eneo hilo waliloishi hapo kwa amani,
anasema.
Washambuliaji
walifanya mashambulizi kwa kutumia bunduki aina ya Kalashnikov kwa waumini
katika kanisa la Deeper Life Bible Church katika mji wa Otite karibu na Okene.
Mchungaji
wa kanisa hilo ni miongoni mwa waliouawa na wengine wengi walijeruhiwa.
Bwana
Wada ametangaza amri hiyo ya hatari kwa eneo la Okene, Otite na jimbo kuu la
Lokoja.
Mwandishi
wetu anasema shambulio hilo limetokea katika eneo la kusini zaidi kuliko maeneo
ambayo hushambuliwa zaidi na Boko Haram.
Watu
wengi watakuwa na hofu kuona shambulio hilo limetokea eneo la Okene, sehemu
ambayo inakutanisha eneo kuu la waislamu la kaskazini na sehemu kubwa ya
wakristo eneo la kusini.
Mwezi
April vikosi vya usalama vya Nigeria vilivamia kiwanda kinachosadikika cha
kutengeneza mabomu eneo la Okene, na kuwaua wapiganaji wasiopungua tisa
wanaosadikika kuwa wa Boko Haram.
Mwezi
February kundi la Boko Haram lilisema lilishambulia gereza eneo la Kogi kwa
kutumia mabomu na silaha nzito ili kuwatorosha wafungwa 119.
Lakini
mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakifanywa zaidi maeneo ya kaskazini. Kundi
hilo linataka kuweka mfumo wa utawala wa sharia nchi nzima.
0 comments:
Post a Comment