Polisi nchini Malaysia, wanasema kuwa mtoto
mwenye umri wa miaka mitatu alifariki nyumbani kwao wakati familia yake
ikimfanyia tambiko la kumpunga mapepo ambalo halikufanikiwa kama
walivyotarajia.
Kwa
mujibu wa polisi katika jimbo la Penang , kaskazini mwa nchi, waliitwa kwenye
nyumba hiyo baada ya mmoja wa jamaa za mtoto huyo kushikwa na na wasiwasi .
Katika
nyumba hiyo polisi walipata watu wazima wanane ikiwemo mamake mtoto huyo,
mfanyakazi wa nyumbani mwenye uraia wa Indonesia wote wakiwa wamejifungia ndani
ya chumba wakiwa wamemlalia mtoto yule na kujifunika mablanketi.
Watu
hao, walikuwa wamejifunika kwa blanketi wakiwa wanaimba nyimbo kwa
kurudiarudia. Kulingana na polisi, kitendo hicho inaarifiwa kilikuwa kimedumu
kwa muda mrefu.
0 comments:
Post a Comment