Wednesday, February 13, 2013
0
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa Benedict wa kumi na sita amewashukuru waumini kwa maombi yao kwake katika hotuba yake ya kwanza hadharani tangu....
 
 kutangaza kuwa anajiuzulu
Papa alishangiliwa na maelfu ya watu alipokuwa anajianda kutoa hotuba yake ya kila wiki mjini Vatican.
Alisema anajiuzulu kwa sababu anaelewa fika kuhusu hali yake ya kiafya inavyoendelea kudhoofika na anavyoishiwa na nguvu kutekeleza majiku yake.
Baadaye leo ataongoza misa yake ya mwisho katika kanisa ya St Peter's Basilica.
Tangazo la kujizulu alilitoa mwishoni mwa Februari,
Papa mwenye umri wa miaka 85, na ambaye jina lake kamili ni Kadinali Joseph Ratzinger ataendelea na majuku yake kama kawaida hadi siku atakapojiuzulu rasmi.
Katika muda wa wiki sita zijazo, Papa mpya anatarajiwa kuteuliwa.
Akiwa na umri wa miaka 78, kadinali Joseph Ratzinger, alikuwa mmoja wa Papa wazee zaidi kuwahi kuteuliwa kuongoza kanisa
Alichukua wadhifa wake wakati ambapo kanisa lilikuwa linakumbwa na kashfa nyingi ikiwemo visa vya kuwaharibu watoto vilivyofanywa na makasisi wa kanisa hilo.



0 comments:

Post a Comment

MAONI YAKO HAPA

Name

Email *

Message *

MARAFIKI

WANAO NITEMBELEA