Askofu wa zamani wa Durham Justin
Welby atakuwa askofu mkuu wa 105 wa Canterbury katika ibada itakayofanyika
katika kanisa kuu la St Paul's Cathedral hii leo, baada ya
kupitishwa kisheria
na tume ya uteuzi iliyomchagua mwaka jana.
Askofu Welby anachukua nafasi ya Dr
Rowan Williams, ambaye aliondoka madarakani mwishoni mwa mwezi wa Desemba na
kuchukua nafasi ya uongozi wa chuo cha Magdalene cha Cambridge.
Mwandishi wa BBC wa masuala ya
kidini Robert Pigott anasema kuwa , zilizokuwa ni taratibu za kisheria tu sasa
zimegeuka kuwa sherehe za ibada ya kanisa kwa kiongozi mpya wa kanisa la
England.
Iwe kwa kiwango na kiroho
kuidhinishwa kwa kutawazwa kwa askofu mkuu wa Canterbury' ni tukio la kipekee.
Maaskofu wakuu watakuwa katika
kanisa la St Paul huku mahakama ya sheria ikitumiwa kufafanua lugha tamu
kuelezea cheo atakachokuwa nacho Justin Welby katika wadhfa wake mpya. Sherehe
na cheo hicho hubadilishwa baada ya karne kadhaa .
Sherehe nyingine za kuvutia kwa
ajili ya Askofu Webly zinazotarajiwa kupambwa na muziki maalum wa kanisa hilo
zitafanyika mwezi ujao katika kanisa kuu la Canterbury .
Hata hivyo , Justin Welby aliomba
kuwa sherehe za leo zifanyike kwa ibada kamili , zikiwemo nyimbo za ibada , ili
kuonyesha umuhimu wa kidini wa sherehe za kutawazwa kwake kwa kiti hicho kipya
.
Wakati askofu mkuu wa York John
Sentamu atakapokuwa akisoma na kuweka ishara za kutawazwa kwake, askofu Welby
atakuwa askofu mkuu wa , na kiongozi wa kiroho wa waumini wapatao milioni moja
wa kanisa la kianglikana duniani
|
0 comments:
Post a Comment