Israel imesema kwamba Waisraeli
watatu wameuwawa na kombora lililofyatuliwa kutoka Ukanda wa Gaza.
Inasema kombora hilo liliangukia
jengo moja la ghorofa la makaazi mjini....
Kiryat Malachi, kusini mwa Israel.
Awali, inasemekana Wapelestina
watatu waliuwawa katika shambulizi la ndege za jeshi la Israel dhidi ya Gaza.
Mwandishi wa BBC aliyeko Gaza
anasema kuwa aliona moshi wa makombora yanayorushwa.
Mashambulizi haya yametokea baada ya
Israel kumuua kiongozi mmoja wa kijeshi wa Hamas, Ahmed Jabari, pamoja na watu
wengine 10 Jumatano.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
lakutana
Nalo Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
limefanya mkutano wa dharura mjini New York ili kujadili mapigano hayo.
Rais wa baraza hilo, Hardeep Singh
Puri wa India, alisema kwamba ni sharti mapigano hayo yakomeshwe mara moja.
Nchi za Kiarabu zilitaka baraza hilo
liishtumu Israel, lakini Marekani ikasema kuwa Israel ilikuwa na haki ya
kujihami dhidi ya makombora yanayorushwa na Wapelestina.
Eud Barak, waziri mkuu wa Isarel |
0 comments:
Post a Comment