Jeshi la Nigeria linasema kuwa
polisi watatu wameuawa katika mashambulizi yaliyofanyika usiku kucha dhidi ya
kituo cha polisi Kaskazaini Mashariki mwa nchi.
Msemaji wa polisi alielezea kuwa
makanisa matatu pamoja na shule moja ya msingi....
ziliteketezwa wakati wa
shambulizi hilo mjini Buni Yadi katika jimbo la Yobe.
Aliongeza kuwa wavamizi waliiba
silaha kutoka kwa kituo hicho cha polisi.
Haijulikani nani aliyefanya
shambulizi hilo ingawa kundi la Boko Haram limekuwa likifanya mashambulizi ya
mara kwa mara Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
0 comments:
Post a Comment