Huku timu za Afrika zikilazimika kusafirisha
mamilioni ya dola za kimarekani hadi Brazil (Nigeria Cameroon)
ilikuzima migomo kabla ya mechi muhimu timu ya Ugiriki ilifanya kinyume
na hayo ilipokataa katakata kupokea malimbikizi ya marupurupu yao kutoka
kwa serikali .
Timu hiyo iliyoondolewa na Costa Rica katika
mkondo wa pili ilimwandikia waziri mkuu wa Ugiriki Antonis Samaras barua
ikimtaka atumie fedha hizo kujenga uwanja mpya wa kandanda utakaotumika
kutambua na kukuza vizazi vipya vya kandanda.Bwana Samaras aliahidi kutekeleza ombi la wachezaji wake alipozungumza kwa njia ya simu na maafisa wa shirikisho la soka la Ugiriki.
0 comments:
Post a Comment