Shirika hilo ambalo huwasaidia waathiriwa wa ubakaji umewafanyia uchunguzi wanawake 34. Ubakaji umekuwa ukitumika kwa miaka mingi kama silaha katika vita vya mashariki mwa DRC lakini shirika la ''Freedom from Torture'' linasema kuwa sasa wanawake magerezani kote nchini humo wanabakwa kama njia moja ya kuwaadhibu na kuwanyamazisha kutozungumza au kuchangia siasa za nchi hiyo.
Wanawake hao waliofanyiwa uchunguzi wanajumuisha wachuuzi, wasomi na hata wataalamu mbali mbali kati ya miaka 18 na 62 kote nchini humo.
Takriban hao wote walitiwa nguvuni kwa kujihusisha na masuala ya haki za binadamu au kampeini za kisiasa, au hata jamaa katika familia yao alihusika na siasa.
Zaidi ya nusu ya wanawake hao wanasema wamebakwa na magenge hata wanaofika kumi. Shirika hilo sasa linataka serikali ya DRC kufanya hima kutekeleza azimio la umoja wa mataifa dhidi ya kuwatesa watu.
0 comments:
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.